Zechariah 6:1-4

Maono Ya Nane: Magari Manne Ya Vita

1 aNikatazama juu tena: nikaona mbele yangu magari manne ya vita yakija kutoka kati ya milima miwili, milima ya shaba! 2 bGari la kwanza lilivutwa na farasi wekundu, la pili lilivutwa na farasi weusi, 3 cla tatu lilivutwa na farasi weupe na gari la nne lilivutwa na farasi wa madoadoa ya kijivu, wote wenye nguvu. 4 dNikamuuliza malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Hawa ni nani bwana wangu?”

Copyright information for SwhKC